Se ha denunciado esta presentación.
Se está descargando tu SlideShare. ×

Zumm A4 Leaflet - Swahili

Anuncio
Anuncio
Anuncio
Anuncio
Anuncio
Anuncio
Anuncio
Anuncio
Anuncio
Anuncio
Anuncio
Anuncio
Cargando en…3
×

Eche un vistazo a continuación

1 de 4 Anuncio

Más Contenido Relacionado

Anuncio

Zumm A4 Leaflet - Swahili

  1. 1. Zungumza na Mtoto Mchanga Talk to Your Baby Taarifa ya Utafiti na Ujuzi Uliotokana na Utafiti 2013 – 2015 Wakusanya taarifa wakijifunza jinsi ya kutumia Kipimo cha Uelewa wa Lugha. Baba huyu alihudhuria mafunzo ya kujengewa uwezo pasipo kudhamiria, lakini sasa anajisikia kuona fahari kwa ajili ya mwanae, na akaondoka akiwa amembeba huku wakiendelea kuongea. Angalia tofauti kati ya mama na mtoto baada ya saa moja tu ya mafunzo kuhusu jinsi ya kuzungumza na mwanae mchanga. 2 Page Folder Leaflet A4 Swahili version.indd 1 01/12/2015 08:29
  2. 2. Zungumza na Mtoto Mchanga Mambo ya Msingi wa jambo hili Mfumo wa Utafiti Upoushahidiwenyenguvukimataifakuhusiananasualalaumuhimu wa mazingira yenye tija ya kukuza vipaji vya lugha katika mwaka wa kwanza wa uhai wa mtoto. Watoto wanaozungumzishwa sana kwa njia sahihi tangu wanapozaliwa hujifunza kuongea mapema, piakuongeavyema. Watoto,wanaojuanakuelewamanenomengi na kuongea mapema wana uelekeo wa kupata mafanikio katika kujifunza kusoma na kuandika pindi wapelekwapo shuleni. Ushahidi wa yale watu waliyotuambia kwa upande mmoja, na mitazamo ya wana taaluma wenzetu kwa upande mwingine, pamoja na yale tuliyoweza kuyabaini katika medani za utafiti, yote haya yanachangia kubainisha kwamba mazingira ya uelewa wa lugha kwa watoto wa Kitanzania si ya kiwango cha juu sana kwa kadiri ilivyopaswa iwe. Ni kana kwamba kwa jumla, wazazi hawazungumzi sana na watoto wao wawapo bado wachanga na wala hawajui umuhimu wa kulifanya jambo hili. Kundi la washika dau takribani 24 kutoka Serikalini pamoja na wadau wengine wa maendeleo walikutana mwishoni mwa mwaka 2011 ili kuamua ni nini kifanyike; na hapo ndipo ilipoamliwa kwamba hatua ya kwanza itakuwa ni kufanya utafiti wa kitaalamu. Huu ni utafiti wa kwanza wa mazingira ya lugha kwa watoto wachanga katika nchi za Kiafrika zilizo kusini ya jangwa la Sahara. Maswali ambayo utafiti huu ulilenga kuyatafutia majibu yalikuwa kama ifuatavyo: • ‘Mazingira ya lugha kwa watoto wachanga nchini Tanzania hasa katika mwaka wa kwanza wa uhai wao yakoje?’ • ‘Ni kwa njia gani, kama inawezekana, mazingira ya lugha kwa watoto wachanga yaboreshwe, kwa namna itakayoongeza uwezo wa kielimu kwa watoto wachanga na hatimaye watoto kwa jumla?’ Mnamo mwaka 2012, utafiti wa awali ulifanyika katika wilaya za Moshi vijijini na visiwa vya Chole na Mafia. UBS Optimus, ambayo ni wakfu wa banki katika nchi ya Switzerland ulitoa fuko la fedha lililotosheleza kufanyika utafiti katika maeneo makubwa, na kwa hiyo malengo ya utafiti yaliboreshwa kutokana na matokeo ya utafiti wa awali. Kibali kutoka COSTECH kilitolewa mwaka 2013, ili utafiti wa majaribio ufanyike katika kaya takriban 1,000 kutoka katika Wilaya tano zilizopatikana kwa kubahatisha pasi na kuzingatia vigezo vyovyote. Mfumo wa utafiti waweza kuonekana katika Jedwali 1. Watafiti wasaidizi wa Kitanzania walikusanya taarifa kutoka katika mazingira ya ndaniyakaya,waalimukatikamaeneoutafitiulipofanyikawaliongozawarshazakuwajengeauwezowatuwafamiliazilizoshirikiutafiti,na Hatua Shughuli Hatua 0 Familia zenye watoto wachanga zinaandikishwa katika makundi mawili tofauti lakini katika jamii zinazofanana kabisa, jamii zilizo katika wilaya 5 tofauti; jamii kwa mtindo wa kubahatisha zinapewa jukumu la kuwa aidha‘Kundi Linaloachiliwa’au‘Kundi Linalojengewa Uwezo’.Wazazi wanaambiwa kwamba ni utafiti unalenga kupata ujuzi wa maendeleo ya mtoto; pasipo kuambiwa kiini cha utafiti wenyewe ili kuepuka uwezekano kuathiri matokeo ya utafiti kwa namna yoyote ile. Hatua 1 Wakusanya taarifa wanazitembelea familia zote zinazohusika katika utafiti mara 3, katika kila safari wakihesabu maneno yanayozungumzwa kwa mtoto katika kipindi cha dakika 30 Utafiti wa KAP (Ujuzi, Mtazamo & Utendaji) hukamilishwa katika safari ya 3 kwa kumwuliza mama wa mtoto mchanga maswali. Hatua 2a Familia zilizo katika kundi linalojengewa uwezo hupewa mafunzo ya kujengewa uwezo ya masaa 2 mara 3 wakiwa katika makundi yanayofikia watu 30 (watu 3 kutoka katika kila familia hualikwa kuhudhuria mafunzo). Kundi linaloachiliwa huachwa. Hatua 3 Wakusanya taarifa huzirudia tena familia na kufanya tena hesabu za maneno mara 3, na utafiti wa pili wa KAP Hatua 4 Wakusanya taarifa huzirudia tena familia zote watoto wanapofikia umri wa miezi 20-24 na kuwapima watoto kwa kipimo rahisi uelewa wa lugha Hatua 2b Familia katika jamii za makundi yanayoachiliwa yanapewa mafunzo ya kujengewa uwezo kwa sababu za kimaadili, lakini hii ni baada ya ukusanyaji taarifa wote kuwa umekamilika Hatua 5 Taarifa zinafanyiwa mchanganuo, tamatishi zinafanyika, taarifa zinaandikwa na kutolewa Jedwali1. 2 Page Folder Leaflet A4 Swahili version.indd 2 01/12/2015 08:29
  3. 3. Zungumza na Mtoto Mchanga Matokeo Unapochanganua taarifa zenye matokeo yasiyolingana (yanayotofautiana), njia bora ya kufuata ni kuchukua viwango vya wastani au vya kati badala ya viwango halisi vinavyoonekana. Thamani ya kati au wastani inawakilisha kiwango cha chini kilichopatikana kwa nusu ya vyanzo vya taarifa, na hiyo itakuwa taarifa ambayo haijaathiliwa na idadi ndogo ya vyanzo vilivyoonyesha matokeo ya juu. Jambo kubwa lililogunduliwa, kama inavyoonyeshwa katika Jedwali 2 ilikuwa kwambamazingirayalughayalikuwahafifu sana katika vikundi vyote, ikiwa pamoja na ukweli kwamba watoto wachanga walizungumzishwamanenomachachesana katika mwaka wao wa kwanza wa uhai. Utafiti wa KAP ulibainisha kwamba wazazi walikuwanauelewamdogosanakuhusiana na umuhimu wa kumzungumzisha mtoto tangu anapozaliwa, na namna hasa inayofaa kwa kumzungumzisha mtoto. Wazazi huongea zaidi na watoto kadiri wanavyokua na kuwa na uwezo wa kuitikia, kwa hiyo tungeweza kutarajia kuongezeka katika idadi ya maneno yanayozungumzwa kwa kila saa (mks) katika kundi lile ambalo halikupewa mafunzo na miongozo ya lugha kwa watoto wachanga katika kipindi cha kwanza cha kuhesabu maneno (umri wa miezi 9) na cha pili (umri miezi 19),pasi na mafunzo yoyote. Kundi Lililoachiliwa lilionyesha nyongeza ya maneno kutoka mks 58 hadi mks 106, ambayo ni nyongeza ya asilimia 83%. Kwa msingi wa nyongeza hii ya asili, tungetegemea nyongeza katika Vikundi vilivyowezeshwa ikue kutoka mks 65 ambayo ndiyo kiwango chao cha chini hadi mks119. Hata hivyo, nyongeza kwa kundi hili ilikua hadi kufikia kiwango cha mks171.Hiiinawakilishanyongezayaziada yaasilimia44%nyongezainayoakisifaidaya mafunzo ya kujengewa uwezo yaliyotolewa kwa familia husika. Viwango hivi, hata hivyo, vimeonyesha faida za warsha za kuzijengea familia uwezo katika hali iliyo hafifu kwa sababu matokeo ya viwango vya watoto ambao wazazi wao walishindwa kuhudhuria warsha za mafunzo ya kujengewa uwezo yameathiri matokeo ya jumla. Kwa maneno mengine ilishindikana kuzitenga familia zilizoshindwa kuhudhuria warsha baada ya kuwa zimeteuliwa. Katika kupima ili kujua ni kiasi gani cha lugha mtoto angeweza kukielewa, tuliweza kuona kwamba katika maeneo ya Kundi Lililoachiliwa kiwango cha wastani au cha kati kilikuwa13/80, wakati kiwango cha kati au wastani katika Kundi Lililojengewa Uwezo kilikuwa bora zaidi kwa asilimia 77%, ambapo kiwango chao cha wastani kilikuwa 23/80. Mambo kadhaa ya faida yalipatikana kutokana na utafiti wa KAP: kwa mfano, ilikuwa bayana kwamba kile wazazi walichojifunza kuhusu kuongea na watoto kilitokana na maonyesho yaliyofanywa na kisha wazazi nao wakafanya kwa vitendo kile walichojifunza katika maonyesho. Walijifunza kwa kutenda kuliko walivyojifunza kwa kupewa habari za kitaalamu. Licha ya taarifa, simulizi kadhaa zilikusanywa na timu za utafiti. Familia zilizo nyingi zilitaarifu kwamba walipowazungumzisha watoto, watoto wao walikuwa wenye furaha, na pia kina baba walianza kuwa na ukaribu na watoto wao wachanga walipoona jinsi watoto wanavyokuwa na mwitikio chanya katika suala la lugha. “Ndiyo, tunaongea na watoto wetu wachanga....lakini hasa pale wao wanapoanza kutuongelesha”(mzazikijana,kablayakupewa mafunzo) “Ninaowatotowatano,lakinikwelininampenda huyuhapa”(baba,baadayakujifunzakuongea namwanaewamwisho) “Nikiongea na mtoto wa miezi 6, ninajiongeresha mwenyewe!” (mama, kabla ya kupewamafunzo) “Hatujawahi kuona mtoto mwenye akili kama huyu” (mzee, baada ya ZUMM kufika kijijinikwao) kazi ya utafiti katika maeneo husika iliendeshwa na Asasi shiriki zisizo za Kiserikali zinazoshughulikia maendeleo ya awali ya mtoto. Mradi kwa jumla uliendeshwa na shirika la Children in Crossfire, asasi isiyo ya Kiserikali iliyosajiliwa nchini Uingereza yenye makao yakeJijini Dar es salaam. Janet na David Townend ambao ndio Waanzilshi wa shirika la ZUMM, waliandaa mfumo wa utafiti, walitayarisha nyaraka na vitendea kazi vilivyotumika katika utafiti, walifanya kazi kwa ukaribu wakishirikiana na mtafsiri wa nyaraka, waliwatembelea wadau mara kadhaa ili kutoa mafunzo kwa timu za wakusanya taarifa na wawezeshaji wa utafiti. 2 Page Folder Leaflet A4 Swahili version.indd 3 01/12/2015 08:29
  4. 4. Tamatishi na hatua zitakazofuata Shukrani Idadiyamanenoyaliyozungumzwakwawatotoyaliongezekakadiri siku zilivyoongezeka katika makundi yote mawili, kama ambavyo ingeweza kutarajiwa kwamba watoto wanavyokua ndivyo wanavyokuwa na mwitikio mzuri. Lakini wale waliohudhuria mafunzo walionyesha kuwa na ongezeko kubwa zaidi la maneno kuliko watoto katika Kundi Lililoachiliwa. Uelewa wa lugha wa watotoambaowazaziwao walipewamafunzo ulikuwa naviwango vya ubora zaidi kuliko watoto katika Kundi Lililoachiliwa. Wazazi nchini Tanzania hutumia maneno machache zaidi kuliko katikanchinyingineyoyoteambakohesabuyamanenoimefanyika. Kiwango cha chini cha mks 63 kinachozungumzwa kwa watoto wachanga ni cha chini mno ukilinganisha na viwango vya maneno kwa saa vinavyopatikana katika tafiti kama hii katika nchi zilizoendelea: mks 600-800 katika familia maskini na hadi kufikia kiwango cha hadi mks 2,000 katika familia za wale wenye ukwasi. (Kwa kulinganisha, watu huzungumza takriban maneno 120 kwa dakika) Matokeo haya yanaonyesha kwamba upo umuhimu kwa ujumbe wa ZUMM kuifikia jamii hasa tunapozingatia umuhimu wa ujuzi wa lugha wa awali katika matokeo ya ujuzi wa kusoma na wa kielimu katika siku za baadaye za mtoto. Habari njema ni kwamba kikwazo kikubwa kinachowazuia wazazi wasiongee na watoto wao wachanga ni hali ya kutojua namna ya kuongea na watoto wao wachanga, na pia kutojua kama upo umuhimu wa kufanya hivyo. Mara wazazi wanapoambiwa ukweli wa jambo hili na kuonyeshwa namna ya kuzungumza na watoto wao wachanga, wengi wao hubadili tabia au mwenendo wao. Kwa kuwa mtoto naye humlipa mzazikwakuitikiakwatabasamunasautizafuraha,tabiahiimpya huendelea na kukua na mara nyingi kuenea hadi katika familia nyingine za jamii husika. Sasa tunao ushahidi wa kutosha kutuwezesha kuzitendea kazi jumbe za ZUMM kupitia mfululizo wa jitihada zitakazoilenga jamii chini ya mwavuli utakaojulikana kama ‘ZUMM kwaVitendo’. ZUMM na CiC ni wadau washirika katika sehemu za utangulizi za mradi huu, mradi utakaotoa mafunzo ya kuwajengea uwezo kwa njia ya mtandao na pia kuwapa vitendea kazi wataalamu walio katika taaluma hii ili waweze kuchukua jumbe za msingi za ZUMM na kuzieneza kwa jamii NchiniTanzania. Kinachohitajika sasa ni kuufikisha ujumbe wa ‘Zungumza sana na mwanao mchanga katika njia sahihi tangu anapozaliwa’, kwa wazazi na familia kote nchini. Haikughalimu kitu kwa wewe kuongea na mtoto wako mchanga; ni jambo ambalo hata wazazi walio maskini sana waweza kulifanya ili kuongeza uwezekano wa majaliwa mema ya watoto wao maishani. ZZUMM na CiC wanashukuru kwa msaada wa Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto, na Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii kwa juhudi zilizofanywa na wizara hizo katika kuruhusu na kuupa utafiti huu jukumu teule.Wanapenda pia kuwapa washirika wao wote wa hapa Nchini shukrani nyingi kwa kazi yao ngumu, pia bila kusahau tunachukua fursa hii kuwashukuru kipekee UBS Optimus kwa msaada wao wa kifedha uliowezesha kufanikisha utafiti huu. Kwa habari zaidi kuhusu ZUMM nenda katika tovuti: www.childrenincrossfire.org/programmes/talktoyourbaby or email jantownend@gmail.com Kwa habari zaidi kuhusu CiC nenda katika tovuti: www.childrenincrossfire.org Maneno yazungumzwayo kwa mtoto kwa saa Kipimo cha Uelewa wa Lugha Angalizo: CG = Kundi achiliwa IG = Jengewa Uwezo Kiwangocha chini Maendeleo %Ongezeko toka kiwangocha Chinihadi Maendeleo Alama/80 Uwiano IG/CG Watoto wote wastani 63 133 111 18 Watoto wote CG/IG Ulinganifu CG wastani 58 106 83 13 1.8 IG wastani 65 171 163 23 Jedwali2. 2 Page Folder Leaflet A4 Swahili version.indd 4 01/12/2015 08:29

×