Se ha denunciado esta presentación.
Se está descargando tu SlideShare. ×

JARIDA LA SHUJAA.pdf

Anuncio
Anuncio
Anuncio
Anuncio
Anuncio
Anuncio
Anuncio
Anuncio
Anuncio
Anuncio
Anuncio
Anuncio
ULIMWENGU WA SIKOSELI . AFYA
MAISHA NA MATUKIO . BURUDANI
SHU AA
JARIDA LA
J
Arafa
Na Arafa Said & Emmy Mwita
ULIMWENGU
WA SIKOSELI
01
|
MAUDHUI
|
|
03
MATUKIO
02
JARIDA LA SHUJAA
SHU AA
JARIDA LA
J
Arafa
Na Arafa Said & Emmy Mwita
...
MHARIRI
|
UJUMBE WA MHARIRI:
“Sikoseli sio ugonjwa wa kurogwa” hayo ni maneno ya Bi. Fatuma Ubwa, Jarida la Shujaa ni ndot...
Anuncio
Anuncio
Anuncio
Anuncio
Próximo SlideShare
CHF Case Study
CHF Case Study
Cargando en…3
×

Eche un vistazo a continuación

1 de 24 Anuncio

JARIDA LA SHUJAA.pdf

Descargar para leer sin conexión

*UTANGULIZI, JARIDA LA SHUJAA*

Kufika kilele cha maadhimisho ya siku ya sikoseli duniani, Taasisi isiyo ya kiserikali ya Sickle Cell Disease Patients Community of Tanzania iliona vyema uhitaji wa kuwepo na Jarida la Sikoseli kwani uwasilishi wa taarifa pekee hautoshi mahitaji ya walengwa, tuliona uhitaji wa kuwepo chombo ambacho kitakuwa ni jukwaa la kutoa elimu na uelewa juu ya sikoseli kwa lengo kuu la kuleta ufahamu zaidi wa sikoseli kwa wanajamii. Ndio, unaweza kuhoji kuwa kwanini jarida hili? ilhali kuna majarida mengi ya afya tayari, na tunaweza kukujibu, kuwa Jarida ili ni muhimu kwani, litakuwa ni chombo muhimu kwa wanajamii wa Sikoseli Tanzania kwa kuwapa nafasi ya kujenga hoja mbalimbali zinahusu ugonjwa wa sikoseli, pia litasaidia kuwa chanzo cha Taarifa za Ulimwengu wa sikoseli kwa walengwa, kikubwa zaidi Jarida ili litakuwa ni mwendelezo wa harakati za taasisi yetu katika kueneza elimu na uelewa wa ugonjwa wa Siko Seli.

Kama wahariri wakuu wa Jarida la Shujaa, lengo letu halikuwa elimu na uelewa tu bali pia kuupa kipaumbele ugonjwa wa sikoseli kwani tukiangalia takwimu zinaonyesha kuwa watoto 300,000 uzaliwa na Sikoseli Tanzania kila mwaka na pia katika watoto 1000 wanaozaliwa, mmoja anazaliwa na Sikoseli kila siku, kuongeza hapo kwa mujibu wa Takwimu 20% ya Watanzania wana vinasaba vya ugonjwa wa Siko Seli; Hivyo Jarida hili ni muhimu kwani litamulika ugonjwa wa Siko Seli na changamoto zote zinazohusika na Sikoseli.

Jarida la Shujaa ni kama ndege apazaye sauti katika majira kwa matumaini kuwa jamii itasikiliza na kuelewa kuhusu ugonjwa wa Siko Seli.

Hivyo, basi kama mdau tunachukua nafasi hii kuwaalika katika uzinduzi rasmi wa Jarida La Shujaa, Jarida la Kwanza la Sikoseli Tanzania.
Ni matumaini yetu kuwa utashirikiana nasi katika harakati hizi za maendeleo ya jamii katika kuhakikisha kuwa jamii inapata elimu na uelewa juu ya sikoseli.

Shukrani.

*UTANGULIZI, JARIDA LA SHUJAA*

Kufika kilele cha maadhimisho ya siku ya sikoseli duniani, Taasisi isiyo ya kiserikali ya Sickle Cell Disease Patients Community of Tanzania iliona vyema uhitaji wa kuwepo na Jarida la Sikoseli kwani uwasilishi wa taarifa pekee hautoshi mahitaji ya walengwa, tuliona uhitaji wa kuwepo chombo ambacho kitakuwa ni jukwaa la kutoa elimu na uelewa juu ya sikoseli kwa lengo kuu la kuleta ufahamu zaidi wa sikoseli kwa wanajamii. Ndio, unaweza kuhoji kuwa kwanini jarida hili? ilhali kuna majarida mengi ya afya tayari, na tunaweza kukujibu, kuwa Jarida ili ni muhimu kwani, litakuwa ni chombo muhimu kwa wanajamii wa Sikoseli Tanzania kwa kuwapa nafasi ya kujenga hoja mbalimbali zinahusu ugonjwa wa sikoseli, pia litasaidia kuwa chanzo cha Taarifa za Ulimwengu wa sikoseli kwa walengwa, kikubwa zaidi Jarida ili litakuwa ni mwendelezo wa harakati za taasisi yetu katika kueneza elimu na uelewa wa ugonjwa wa Siko Seli.

Kama wahariri wakuu wa Jarida la Shujaa, lengo letu halikuwa elimu na uelewa tu bali pia kuupa kipaumbele ugonjwa wa sikoseli kwani tukiangalia takwimu zinaonyesha kuwa watoto 300,000 uzaliwa na Sikoseli Tanzania kila mwaka na pia katika watoto 1000 wanaozaliwa, mmoja anazaliwa na Sikoseli kila siku, kuongeza hapo kwa mujibu wa Takwimu 20% ya Watanzania wana vinasaba vya ugonjwa wa Siko Seli; Hivyo Jarida hili ni muhimu kwani litamulika ugonjwa wa Siko Seli na changamoto zote zinazohusika na Sikoseli.

Jarida la Shujaa ni kama ndege apazaye sauti katika majira kwa matumaini kuwa jamii itasikiliza na kuelewa kuhusu ugonjwa wa Siko Seli.

Hivyo, basi kama mdau tunachukua nafasi hii kuwaalika katika uzinduzi rasmi wa Jarida La Shujaa, Jarida la Kwanza la Sikoseli Tanzania.
Ni matumaini yetu kuwa utashirikiana nasi katika harakati hizi za maendeleo ya jamii katika kuhakikisha kuwa jamii inapata elimu na uelewa juu ya sikoseli.

Shukrani.

Anuncio
Anuncio

Más Contenido Relacionado

Presentaciones para usted (20)

Anuncio

JARIDA LA SHUJAA.pdf

  1. 1. ULIMWENGU WA SIKOSELI . AFYA MAISHA NA MATUKIO . BURUDANI SHU AA JARIDA LA J Arafa Na Arafa Said & Emmy Mwita
  2. 2. ULIMWENGU WA SIKOSELI 01 | MAUDHUI | | 03 MATUKIO 02 JARIDA LA SHUJAA SHU AA JARIDA LA J Arafa Na Arafa Said & Emmy Mwita MITINDO YA MAISHA 04 DONDOO ZAAFYA |
  3. 3. MHARIRI | UJUMBE WA MHARIRI: “Sikoseli sio ugonjwa wa kurogwa” hayo ni maneno ya Bi. Fatuma Ubwa, Jarida la Shujaa ni ndoto yetu sote katika jumuiya ya Sikoseli, Kupata nafasi ya kukaribisha dunia yetu kushiriki na kujifunza mengi kuhusu ugonjwa wa sikoseli, Tunapotamka neno, “Ugonjwa” Kila mmoja wetu anakimbilia udhaifu, kama wahariri wa jarida hili la SHUJAA lengo letu kuu ni kuchora picha chanya juu ya sikoseli, ndio maana ukiendelea kusoma jarida hili utaona kuwa kuna stori za mashujaa kama, Aboubakari Kilaza ambaye ni mwanamuziki wa Bongo Flava; ambao wanakupa motisha na kuhimiza kuwa Sikoseli haikuzuii kuishi Maisha ya kawaida na kutimiza ndoto zako. Utakutana na muigizaji wa Bongo Movies Thadeus al-maaruf kama shetani wa mguu mmoja, yeye anatuhimiza kutokata tamaa pamoja na changamoto za kiafya alizopata, hadithi yake ni dhahiri kuwa ni hadithi ya ushindi. | SHU AA JARIDA LA J Arafa Na Arafa Said & Emmy Mwita Ndani ya Jarida pia utajifunza kuhusu afya, mitindo ya Maisha na pia utapata taarifa muhimu kwa yale yanayojiri katika ulimwengu wetu wa Sikoseli. Lengo kuu la Jarida hili ni kuwafungulia dunia wanajamii wa sikoseli kuwawezesha kupata chombo ambacho kitawawezesha kupaza sauti yao na kuufikia ulimwengu kwa ujumla. Tunapenda kutoa shukrani za dhati kwa waandaji wote na timu nzima iliyoshiriki katika kuwezesha jarida hili kukamilika. Ni matumaini yetu kuwa utalipokea na kulisoma kwa mikono miwili jarida hili la SHUJAA. Kuwa Mjanja Ijue Sikoseli. Arafa Salim. Emmy Mwita. _ _
  4. 4. SIKU YA SIKOSELI DUNIANI K 01 | wanza tuelekee Arusha, ambapo kwa mara ya kwanza maadhimisho hayo yaliadhimishwa jijini huko Kitaifa katika Hospitali kuu ya jiji la Arusha ya Mount Meru Referral Regional Hospital; Mgeni Rasmi akiwa Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Afya Dkt. Seif Shekalaghe kwa niaba ya Naibu Waziri Dkt. Godwin Mollel, Jumuiya ya Watu Wenye Sikoseli Tanzania iliwakilishwa na wajumbe wao kutoka Sickle Cell Community group, ambapo walishiriki katika matembezi ya kilomita 1, yaliyoanzia ofisi ya Halmashauri ya Manispaa ya jiji la Arusha na kumalizika katika Hospitali ya Mount Meru; Na baada ya hapo utambulisho na hotuba kutoka kwa Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Afya Dkt. Seif Shekalaghe na wageni muhimu waalikwa, Ikifuatiwa na tukio maalum la uzinduzi wa kliniki mpya ya sikoseli Hospitalini hapo ikiwa ni jambo la kheri kwa watu wenye sikoseli maana watapata huduma kwa ukaribu zaidi na pia itasaidia kuepuka gharama za kuhudhuria kliniki binafsi. Pia maadhimisho hayo yalipambwa na risala na shuhuda kutoka kwa watu wenye sikoseli waliohudhuria ambapo walipata kushirikisha adhara juu ya safari zao kama watu wanaoishi na sikoseli na kutoa hamasa na ufahamu kwa hadhara. Kila mwaka, juni 19 ni siku maalum kwa jamii ya sikoseli duniani kama ilivyoazimiwa na umoja wa mataifa mwaka 2004 kila siku ya tarehe 19 itakua siku ya uhamasishaji na ufahamu wa sikoseli duniani. Hivyo kila mwaka, juni 19, jamii ya kimataifa ya sikoseli inaungana kuadhimisha, kutoa elimu na uelewa juu ya sikoseli. Leo tutatazama yaliyojiri katika maadhimisho ya siku ya sikoseli duniani, nchini Tanzania. Tutaangalia matukio na taarifa kutoka mikoa mbalimbali ambazo ziliadhimisha siku hiyo rasmi ambayo ni Juni 19, 2022. | ULIMWENGU WA SIKOSELI JUNI 19, | SHU AA JARIDA LA J Arafa Na Arafa Said & Emmy Mwita
  5. 5. Kutoka Bara tunavuka bahari hadi visiwani Zanzibar ambapo nao hawakuachwa nyuma katika maadhimisho hayo kwani siku ya Tarehe 17 Juni 2022 waliadhimisha siku ya sikoseli duniani katika Hospitali ya rufaa ya Mnazi Mmoja Zanzibar, Maadhimisho hayo yalifana huku yakiwaleta pamoja wana jumuiya wote wa Sikoseli kisiwani hapo pamoja na watoa huduma za afya. | | | | SIKU YA SIKOSELI DUNIANI 01 | ULIMWENGU WA SIKOSELI JUNI 19, | SHU AA JARIDA LA J Arafa Na Arafa Said & Emmy Mwita
  6. 6. | K utoka Zanzibar tunaelekea hadi Pwani, Bagamoyo ambapo Sickle Cell Disease Patients' Community of Tanzania iliandaa maadhimisho ya siku ya sikoseli duniani kushirikiana na hospitali ya wilaya ya Bagamoyo, siku ya Tarehe 25 Juni, 2022. Maadhimisho hayo yaliyofanyika katika viwanja vya Shule ya Msingi Mwambao, wilayani Bagamoyo; Mgeni rasmi akiwa Mheshimiwa Kaimu Mkurugenzi wa Wilaya ya Bagamoyo Bw. Majid Mhina. Sherehe hizi zilifana kwa burudani kutoka kwa vikundi vya waaigizaji na wasanii wa ngoma za asili Bagamoyo pamoja na Elimu ya somo la Lishe Bora kutoka kwa mtaalamu wa Lishe na Afya Bora; ikifuatiwa na hotuba kutoka wa mgeni rasmi Kaimu Mkurugenzi Wilaya ya Bagamoyo Bw. Majid Mhina na uzinduzi rasmi wa kliniki ya sikoseli wilayani Bagamoyo. Ziada ya hayo kulikuwa na upimaji wa uviko pamoja na elimu ya afya ya kinywa kutoka Colgate, vilevile ugawaji wa kitabu cha Amana Shujaa wa Sikoseli kilichoandikwa na Bi. Arafa Said huku tukio hilo likiambatana na ushuhuda kutoka kwa shujaa mwenye umri wa miaka 70, akieleza ni jinsi gani ameweza kuishi na kustahimili adha za ugonjwa huo hadi kufikia miaka hiyo 70 huku akivunja Imani potofu za kuwa mtu mwenye sikoseli hawezi kuishi zaidi ya miaka mitano au kupata mafanikio katika Maisha. Tafrija hizi zikiwa ni kilele cha maadhimisho ya sikoseli duniani nchini Tanzania, zillfika kikomo mida ya jioni. | | | | | SIKU YA SIKOSELI DUNIANI 01 | ULIMWENGU WA SIKOSELI JUNI 19, | SHU AA JARIDA LA J Arafa Na Arafa Said & Emmy Mwita
  7. 7. SERIKALI YAWAFUTA MACHOZI YA MIAKA MINGI WATU WAIISHIO NA SIKOSELI ama umewahi kusikia au unafahamu kuhusu dawa ya hydroxyurea utakuwa pia unatambua umuhimu wake kwa watu wenye sikoseli katika kuhakikisha kuwa wanaishi Maisha yenye ubora na afya kwa kupunguza dalili hatarishi zinazosababishwa na ugonjwa wa sikoseli.Hivi karibuni katika kongamano la Kisayansi lililofanyika Chuo Kikuu cha Afya na Sayansi Shirikishi Muhimbili (MUHAS), Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya, K Prof. Abel Makubi akiwa mojawapo ya wageni rasmi aliahidi kushughulikia suala hilo na kulikamilisha haraka hii ni katika kuhakikisha utekelezaji wa mojawapo ya sera za wizara ya afya Tanzania ikiwa pamoja na kuboresha huduma za afya kwa watu wenye sikoseli nchini. Mheshimiwa wa Katibu Mkuu Wizara ya Afya Prof. Abel Makubi aliagiza hayo wakati alipokiwa anahitimisha kongamano la saba la kisayansi, chuo kikuu cha Afya na Sayansi Shirikishi Muhimbili (MUHAS).Nukuu ya Mheshimiwa Prof. Abel Makubi, “NHIF hakikisheni mnatekeleza hili, hivi vidonge vipatikane kwenye vifurushi vyote vya bima, mnipe majibu mapema mlipofikia, ili tufanye maamuzi” Aliagiza Mheshimiwa wa Katibu Mkuu Wizara ya Afya, Prof. Abel Makubi. Pia Mhe. Katibu Mkuu, Aliongeza kwa kusema kuwa suala hilo, kuhusu upatikanaji wa Hydroxyurea litazamwe na kushughulikiwa kwa uzito kwani Dawa ya Hydroxyurea ni muhimu kutokana na Kwamba watu wengi wenye sikoseli wanaishi katika Maisha ya kupata maumivu mara kwa mara na dawa ya hydroxyurea inawasaidia kupunguza dalili nyingi zingi zinazosaba- bishwa na sikoseli ikiwemo pamoja na kupunguza hali ya kuishiwa damu; na ukosekanaji wa dawa hiyo katika vifurushi vya mfuko wa Afya wa NHIF unawalazimu wanajamii ya sikoseli kulipia gharama ambazo wengi hawa- zimudu kwa ajili ya kupata Hydroxyurea kwa matibabu yao. Mheshimiwa Katibu Mkuu Wizara ya Afya, Prof. Abel Makubi aliongeza kwa kusema, “Tuangalie jinsi ya kusaidia wagonjwa hawa katika hili, hukabiliwa na maumivu makali, wanaishiwa damu lakini dawa hii inawasaidia kuwapunguzia hayo” mwisho wa nukuu. Jarida la Shujaa linatumaini kuwa habari hii ni furaha kwa jamii nzima ya sikoseli kwani baada ya kilio na changamoto za muda mrefu katika upatikanaji wa dawa ya Hydroxyurea sasa wahusika wote wenye Bima ya NHIF wanaweza kupata dawa hiyo bila malipo katika vituo vya Afya; Habari hii inaleta mawanga na matumaini ya kuishi Maisha bora na afya tele bila masumbuko kwa watu wote wenye sikoseli nchini. | | | | |SHU AA JARIDA LA J Arafa Na Arafa Said & Emmy Mwita 01 | ULIMWENGU WA SIKOSELI |
  8. 8. U Pia kutokana na uhaba wa upatikanaji wa huduma za afya na matibabu sahihi kwa wagonjwa wa sikoseli bila kusaha gharama za juu za matibabu, hii inapelekea asilimia kubwa ya watu wenye sikoseli kushindwa kumudu gharama za matibabu katika vituo binafsi na kupelekea kufeli kupata matibabu sahihi hivyo afya zao kuzorota kutokana na athari zinazoletwa na ugonjwa huo hivyo kupelekea wengi wao kupoteza Maisha katika umri mdogo kwasababu ya kukosa uangalizi wa mapema. Kwa miaka mingi jamii ya sikoseli ukijumuisha na wanaharakati wa sikoseli wamekua wakipaza sauti juu ya umuhimu wa upatikanaji wa huduma bora na matibabu sahihi kwa wanajamii ya sikoseli ili kuongeza ubora wa Maisha na afya zao. Hatimaye serikali kushirikiana na washika dau mbalimbali katika sekta ya afya walisikia vilio vyao na toka mwaka 2007 mpaka sasa, kumekua ongezeko la kliniki mpya za sikoseli katika vituo vya afya vya ngazi ya msingi, wilaya na hata Taifa kwa ajili ya uangalizi wa karibu kwa watu wenye sikoseli. Nikiongeza, na kwa mwaka 2022 Jarida letu lingependa kukuhabarisha kuwa sasa wigo wa huduma za afya kwa watu wenye sikoseli unazidi kutanuka na kukukua kwani kuacha kliniki za Mloganzila, Mwananyamala, Temeke na Kliniki iliyopo Hospitali ya Taifa Muhimbili, serikali yetu kupitia wizara ya Afya imeongeza kliniki nyingine mpya, hii ikiwemo Kliniki ya Sikoseli mkoani Kilimanjaro katika Hospitali ya KCMC, tunapenda kuwahabarisha wanajamii wa sikoseli waliopo Moshi, Kilimanjaro kuwa sasa huduma za afya kwao zimesogezwa karibu kabisa, kwani kuna kliniki mpya ya sikoseli, katika jingo la Hemophilia Center, Kitengo cha matibabu ya saratani. Pia bila kusahau kuwa mwezi huu siku ya maadhimisho ya sikoseli duniani, jijini Arusha katika Hospitali ya jiji Mount Meru, Mheshimiwa Naibu Katibu Mkuu katika Wizara ya Afya Dkt. Shekalaghe alizindua kliniki mpya ya sikoseli katika Hospitali hiyo Kongwe, tukielekea mkoani Pwani, Wilayani Bagamoyo napo hawakuwa nyuma katika harakati hizi, Mheshimiwa Kaimu Mkurugenzi wilaya ya Bagamoyo, Pwani alikata utepe na kufungua rasmi Kliniki ya Sikoseli Bagamoyo na Kuagiza kuwa wapewe ushirikiano na Halmashauri ya Wilaya ya Bagamoyo, hii ni pamoja na uangalizi na upatikanaji wa vifaa tiba. Tukifunga kurasa hii, Tunaweza kusema, “Harakati za sikoseli Tanzania, Kumenoga ” Ni matumaini yetu kuwa uwepo wa kliniki hizi utapunguza adha waliyokuwa wakipitia wagonjwa wengi wa sikoseli mikoani nan je ya jiji la Dar es Salaam kwa kusafiri umbali ili kupata matibabu au kulazimika kuhudhuria matibabu katika vituo binafsi hivyo kubeba mzigo mkubwa wa gharama za matibabu na pia hatua hii itapelekea kupunguza vifo vya awali vya wagonjwa wa sikoseli. Shujaa ingependa kuendelea kuwahasa na kusisitiza wanajamii wa sikoseli kuhudhuria kliniki hizi ili kupata matibabu sahihi na endelevu, pia kwa serikali yetu tukufu tunasema, “shukrani na kazi iendelee” | UZINDUZI WA KLINIKI ZA SIKOSELI KWA MWAKA 2022. 01 | ULIMWENGU WA SIKOSELI | SHU AA JARIDA LA J Arafa Na Arafa Said & Emmy Mwita gonjwa wa Sikoseli ni ugonjwa wa kurithi ambao unaathiri seli hai nyekundu za damu na kubadili umbo lake kutoka katika umbo la kawaida la donati na kuipa seli hai nyekundu umbo la ndizi au mundu hii hutokana na upungufu wa oksijeni, protini katika Hemoglobin ya seli; Hivyo hali hii inapelekea mtu kupata dalili kama maumivu makali ya viungo na hata hali ya kupungukiwa damu (anemia). Tafiti zinaonesha kuwa Tanzania ni mojawapo ya nchi zinazoongoza katika chati ya dunia kwa kuwa na asilimia kubwa ya watu wenye sikoseli ikishika nafasi ya nne; Pia tafiti zinaonesha kuwa kila mwaka Watoto 11,000 huzaliwa na sikoseli nchini, Tanzania. Pia makadirio yanaonesha karibu asilimia 20% ya watanzania wanazaliwa na vinasaba vya sikoseli; | |
  9. 9. W WARSHA YA CONSA (CONSORTIUM OF NEWBORN SCREENING IN AFRICA) 02 | MATUKIO | SHU AA JARIDA LA J Arafa Na Arafa Said & Emmy Mwita arsha hii ilifanyika Juni 22, 2022 kuanzia saa tatu asubuhi mpaka saa tisa alasiri katika ukumbi wa kampasi ya chuo cha MUHAS; Ilijumuisha watoa huduma ya afya pamoja na kitengo cha Sikoseli MUHAS, wazazi wote ambao wana watoto wenye Sikoseli na waliogunduliwa kupitia kipimo cha Newborn Screening. Lengo la warsha hiyo likiwa ni kutoa elimu kwa wazazi hao kupitia matabibu wenye ujuzi na weledi wa juu; Pia kuacha elimu ya malezi kwa Watoto wenye Sikoseli walitoa elimu juu ya umuhimu wa kuwa na bima ya Afya ya NHIF ili kuwawezesha kupata huduma zote muhimu za matibabu na kliniki kwa Watoto hao hivyo kuwapunguzia mzigo wa gharama za kulipia kwa njia ya fedha. Kuacha elimu iliyotolewa na wataalamu wa afya waalikwa, wazazi walipata nafasi ya kueleza jamii juu ya safari zao kama wazazi wa Watoto wenye Sikoseli na waliogundulika katika umri mchanga na pia wazazi hao walieleza jinsi safari hii ina milima na mabonde mengi na vile kuwa na mtoto mwenye mahitaji maalum ni safari ya kuwa na Subira, upendo na kuwa tayari kujifunza kila siku na kushirikiana na asasi zilizopo na watoa huduma ili kuhakikisha malezi ya mtoto yanapewa kipaumbele na anapata matibabu na huduma sahihi za afya kwa ukuaji mzuri. Huduma za vipimo vya Newborn Screening zinapatikana katika vituo vya afya vya Amana, Temeke, Muhimbili na Bugando nchini, Tanzania.
  10. 10. K KONGAMANO LA SABA LA KISAYANSI, CHUO KIKUU CHA MUHAS. 02 | MATUKIO | SHU AA JARIDA LA J Arafa Na Arafa Said & Emmy Mwita ongamano la saba la kisayansi lililoandaliwa na wanazuoni na wataalamu wa tiba na sayansi wa chuo kikuu cha Afya na Sayansi Shirikishi Mhumbili (MUHAS) na Kufanyika chuoni hapo siku ya Tarehe 26, Januari 2022 katika Kampasi kuu ya Dar-es-salaam; Lengo kuu ikiwa ni kujadili mwelekeo mpya wa nchi katika kukabili ugonjwa wa sikoseli ambao unaathiri asilimia kubwa ya Watoto nchini, Tanzania. Kongamano ilo lilishirikisha na kukutanisha washika dau mbalimbali katika sekta ya Afya na Sayansi, likijumuisha Wizara ya Afya, wanazuoni na wakufunzi mbalimbali, watafiti katika sekta ya Afya, watoa huduma na Mfuko wa Bima ya Afya NHIF pamoja na wengineo wengi. Mojawapo ya mambo yaliyozungumziwa ilikuwa ni pamoja na utekelezaji wa sera ya bima ya afya pamoja na kujumuisha dawa ya Hydroxyurea katika vifurushi vya mfuko wa Bima ya Afya Taifa, NHIF kwa faida ya wagonjwa wa sikoseli nchini. Dkt. Agnes Jonathan, Daktari Bingwa wa Afya ya Jamii pamoja na kuwa Mratibu wa Mradi wa Sikoseli (SPARCO, TANZANIA) MUHAS katika uwakilishi wake wa mada juu ya sikoseli alisema, tafiti zinaonesha kuwa kadiri ya Watoto 11,000 huzaliwa na ugonjwa wa sikoseli, hivyo yeye kama mratibu wa mradi wa SPARCO, TANZANIA pamoja na timu nzima wamefanikiwa kuwaingiza kwenye mfumo wa Tiba na ufuatiliaji wa karibu katika matibabu ya kliniki ya sikoseli takribani Watoto 5000 na pia wamewapatia vitabu ambavyo vinabeba taarifa zao muhimu za afya. Dkt. Agnes Jonathan, aliongeza kuwa tafiti zinaonesha kuwa takribani asilimia 13 hadi 20 ya watanzania wamebeba vinasaba vya ugonjwa wa sikoseli na asilimia iliyosalia bado hawajui hali zao. Pia mojawapo ya wageni rasmi waalikwa alikua Mheshimiwa Prof. Abel Makubi Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya, ambapo alisisitiza juu ya umuhimu wa hydroxyurea kujumuishwa katika mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya, NHIF kwasababu ya umuhimu wa dawa hiyo kwa watu wenye sikoseli, Pia Mheshimiwa wa Prof. Abel Makubi, Katibu Mkuu Wizara ya Afya aliongeza kwa kusema, “Tanzania inastahili iwe na kituo cha umahiri kwa upande wa sikoseli” mwisho wa nukuu. Taasisi ya Jumuiya ya Wagonjwa wa Sikoseli Tanzania (SCDPCT) nayo haikuachwa nyuma, ikiwakilishwa na Mkurugenzi Mwanzilishi wake, Bi. Arafa Said; Akiwakilisha hoja juu ya umuhimu wa uboreshwaji huduma za afya kwa watu wenye sikoseli Tanzania pia alichukua nafasi hiyo kuwaelimisha na kuzungumza juu ya, “Uzoefu na Maisha ya wagonjwa wa sikoseli” akiwakilisha jumuiya ya wagonjwa wa sikoseli Tanzania. Ni dhati kuwa Kongamano ilo la saba la Kisayansi lililoandaliwa na chuo kikuu cha MUHAS lilikuwa chachu ya mabadiliko katika Tiba na Huduma za Afya kwa watu wenye Selimundu kwani Baada ya hapo, Dawa za Hydroxyurea ziliweza kujumuishwa katika mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya NHIF, na sasa watu wote wenye sikoseli wanaweza kupata dawa hizo bure bila kulipa gharama yeyote kupitia Bima ya NHIF.
  11. 11. M MAONYESHO YA KAZI YA WANAHARAKATI WA SIKOSELI TANZANIA 02 | MATUKIO | SHU AA JARIDA LA J Arafa Na Arafa Said & Emmy Mwita aonesho ya vikundi vya wanaharakati wa sikoseli Tanzania yalifanyika Tarehe 28 Januari, 2022 katika kituo cha Sickle Cell Centre, MUHAS. Maonesho hayo yaliandaliwa na taasisi isiyo ya kiserikali ya Jumuiya ya wagonjwa wa sikoseli Tanzania (SCDPCT) ikishirikiana na MUHAS Sickle Cell Program. Lengo la maonesho likiwa ni kuwaleta pamoja wanaharakati wa Sikoseli nchini na kuwapa uwanja wa kuonesha kazi zao na ufanisi walio nao katika kuhakikisha elimu na ufahamu juu ya Sikoseli unakuwepo nchini Tanzania. Taasisi ya Jumuiya ya wagonjwa wa Sikoseli Tanzania (SCDPCT) ilipata nafasi ya kuonesha baadhi ya kazi zao katika warsha hiyo ilifanyika katika kituo cha Sikoseli, MUHAS. Mojawapo ya Kazi zetu ambazo tulionesha zilijuimusha vitabu vya SHUJAA na AMANA SHUJAA WA SIKOSELI na machapisho ya elimu ya Sikoseli, hii ikijumuisha toleo la kwanza la kijitabu cha SAUTI YA SHUJAA ambapo ni mjumuisho wa masomo kuhusu mambo mbalimbali ya Afya ambayo yanaathiri wagonjwa wa Sikoseli kwa ujumla. Pia tulipata nafasi ya kuonesha kupitia picha Kampeni na Kazi za Kijamii ambazo Taasisi inafanya ili kueneza elimu na ufahamu wa Sikoseli katika maeneo na mikoa mbalimbali Tanzania. Lengo la kazi hizi zote ni kuhakikisha kuwa elimu na ufahamu juu ya ugonjwa wa sikoseli unafikia watanzania wote na pia wanaharakati wa sikoseli wanapata fursa ya kuonesha kazi zao na kujumuika na jumuiya wa wenye Sikoseli na kujua mahitaji yao ili kuwepo na maboresho kwa kipindi kijacho mbeleni. Maonesho yalifika kilelel na wanavikundi pamoja na waalikwa walipata kujifunza na kuona kazi mbalimbali ambazo vikundi hivyo vya wanaharakati na wajumbe wa jumuiya ya Sikoseli wanazifanya ili kukabiliana na changamoto zilizopo katika jamii juu ya sikoseli na pia ili kuhakikisha dhana potofu zinapotea na kunakuwepo na uelewa, ufahamu na elimu juu ya Sikoseli.
  12. 12. DONDOO MUHIMU ZA KUISHI NA UGONJWA WA SIKOSELI 02 | DONDOO ZA AFYA | SHU AA JARIDA LA J Arafa Na Arafa Said & Emmy Mwita Siko seli/seli mundu ni nini? Siko seli ni ugonjwa wa kurithi unaosababisha mabadiliko yasiyo ya kawaida katika umbo la chembechembe nyekundu za damu. Kwa kawaida chembe nyekundu za damu zina umbo la mviringo ambalo huzirahisishia kupita kwenye mishipa midogo ya damu ili kusafirisha hewa safi ya oxygen katika sehemu mbalimbai za mwili. Kwa mtu mwenye ugonjwa wa siko seli, seli hizi huwa tofauti; zinanata na zina umbo la mwezi mchanga (mundu). Tanzania ni mojawapo kati ya nchi zenye wagonjwa wengi wa siko seli duniani ambapo inakadiriwa takribani watoto 11,000 huzaliwa na ugonjwa wa siko seli kila mwaka. Pia inakadiriwa kuwa 12% hadi 20% ya watu wote nchi wana vinasaba vya ugonjwa wa siko seli (sickle cell trait), kutegemeana na eneo. Dondoo Muhimu za kuishi na ugonjwa wa Siko seli. a. Uchunguzi wa kiafya wa mara kwa mara ni muhimu kwa watoto wa chini ya mwaka mmoja. Wanapaswa kumuona daktari kila baada ya miezi miwili au mitatu b. Watoto kuanzia mwaka mmoja mpaka mitano wanatakiwa kumwona daktari kila baada ya miezi mitatu Kuzuia Maambukizi c. Hakikisha watoto wanapata chanjo zote za kawaida d. Watoto wapewe chanjo ya ziada ya kuzuia kichomi (Pneumococcal vaccine) e. Watoto wote wenye umri chini ya miaka 6 wapatiwe dawa ya penicillin ili kujikinga na maambukizi f. Hakikisha watoto wanakingwa na maambukizi ya malaria kwa kutumia chandarua chenye dawa Zingatia Ushauri wa Kitaalamu g. Watoto wanatakiwa kunywa maji ya kutosha wakati wote na wapewe mlo kamili, ukijumuisha matunda, mbogamboga, vyakula vya kutia nguvu na vya kujenga mwili wa mtoto. h. Watoto waepuke kukaa katika mazingira ya joto kali ama baridi sana i. Watoto wajishungulishe na michezo mbalimbali ili wawe na furaha na afya njema, wasicheze kiasi cha kuwachosha sana.
  13. 13. W UMUHIMU WA LISHE BORA KWA WENYE SIKOSELI 02 | DONDOO ZA AFYA | SHU AA JARIDA LA J Arafa Na Arafa Said & Emmy Mwita agonjwa wengi wa sikoseli wanaweza kuwa na mwili mdogo lakini kuna hatari ya kuwa na unene uliopita kiasi. Wanashauriwa kula vyakula vyenye kalori ya juu na vyenye virutubisho vingi tangu utotoni. Lishe Bora; ni ile ambayo inajumuisha aina zote za vyakula ambavyo vina virutubisho vinavyohitajika mwilini. Ili lishe iwe bora lazima sahani iwe na mjumuisho ufuatao: 1/4 iwe Wanga, 1/4 iwe Protini na 1/2 iwe na vyakula vyenye Vitamini. Sahani yako inatakiwa kuwa na Wanga (ugali, wali,mtama, mhogo, gimbi, viazi, ndizi etc), Protini, Vitamini A, B6, C, D, E na virutubisho vingine vidogo kama zinki, kalsiamu na magnesiamu. Lishe bora ni muhimu katika kuongeza chembe za damu, kuimarisha mifupa, kuupa mwili nguvu na kuongeza kinga ya mwili. Ili kuhakikisha kuwa unapata lishe bora katika mlo wako wa kila siku ni muhimu kuzingatia mambo yafuatayo; Angalau sahani yako iwe na aina 1 ya Protini na mboga na matunda (chakula kimoja kinaweza kuwa na kirutubisho zaidi ya kimoja), kwa wale ambao ni ngumu kuepuka kuongezewa damu mara kwa mara wanashauriwa kupunguza vyakula vyenye madini chuma kwa asilimia kubwa pia unashauriwa kula vyakula vinavyotoka/ vinalimwa ardhini kwa njia ya asili (organic foods) hivyo ni bora zaidi ya vile vya viwandani na vinavyochakatwa kupita kiasi. Bila kusahau umuhimu wa maji katika mmeng'enyo wa chakula, usafirisha virutubisho katika mwili, msukumo mzuri wa damu. Unashauriwa glasi 8 sawa na Lita 2 au 3 kwa siku. Watu wengi wanashindwa kula lishe bora kutokana na kuwa na uhusiano mbovu na vyakula; Lishe bora ni vile unavyopangilia sahani yako na virutubisho utakavyoweka. Makala hii ya Lishe Bora imenukuliwa kutoka katika chapisho la kwanza la SAUTI YA SHUJAA, somo ambalo lilitolewa na Dkt. Victoria Msambichaka, mtaalamu wa lishe kutoka Hospitali ya Taifa Muhimbili. |
  14. 14. “HUU SI UGONJWA WA KUROGWA” 03 | MITINDO YA MAISHA SHU AA JARIDA LA J Arafa Na Arafa Said & Emmy Mwita “Ninaishi na Siko Seli miaka 70 sasa. Nikiwa na miaka 15 nilianza kuugua mara kwa mara, awali haikujulikana tatizo langu nini, nilikuwa naishiwa damu mara kwa mara, nalazwa kuna nyakati pia niliongezewa maji,” anasimulia.
  15. 15. “HUU SI UGONJWA WA KUROGWA” 03 | MITINDO YA MAISHA SHU AA JARIDA LA J Arafa Na Arafa Said & Emmy Mwita “Ninaishi na Siko Seli miaka 70 sasa. Nikiwa na miaka 15 nilianza kuugua mara kwa mara, awali haikujulikana tatizo langu nini, nilikuwa naishiwa damu mara kwa mara, nalazwa kuna nyakati pia niliongezewa maji,” anasimulia. Jamii imegubikwa na dhana nyingi potofu juu ya ugonjwa huu, wengi hukimbilia kwa waganga wa kienyeji wakiamini wamerogwa au kukumbwa na pepo wabaya; Pamoja na hao wapo wengine ambao huamini mgonjwa wa Siko Seli hawezi kuishi zaidi ya miaka 18. Lakini maisha ya Fatuma Ubwa, Mkazi wa Bagamoyo mkoani hapa ni ushuhuda tosha kwamba mtizamo huo si sahihi. Mwanamama huyo Juni, mwaka huu amesherehekea miaka 70 ya kuzaliwa kwake, ni mgonjwa wa Siko Seli. Zaidi anasimulia.... “Nikiwa na miaka 15 nilianza kuugua mara kwa mara, awali haikujulikana tatizo langu nini, nilikuwa naishiwa damu mara kwa mara, nalazwa kuna nyakati pia niliongezewa maji,” anasimulia. Anasema kutokana na hali hiyo wazazi wake walihisi amerogwa na wapo wanajamii ambao walishauri apelekwe haraka kwa wataalamu {waganga wa kienyeji akatibiwe huko}. “Lakini baba yangu alikataa, hivyo niliendelea kupelekwa hospitalini na huko baadae niligundulika nina Siko Seli. Hivyo, nimezaliwa na Siko Seli, naishi nayo kwa miaka 70 sasa.” Anasema amejaliwa kupata watoto wanne ambao wao hawana Siko Seli, vile vile amejaliwa wajukuu kadhaa ambao nao hawana ugonjwa huu. Uso wake umejaa tabasamu, kila anaposimulia simulizi yake wengi huvutiwa na kustaajabu namna gani ameweza kumudu kuishi nao kwa miaka yote hiyo? Anasema wazazi wake walizingatia kumpeleka kliniki kila alipohitajika na kwamba ameishi hivyo akizingatia maelekezo anayopatiwa na wataalamu wa afya. Fatuma anaongeza “Siko Seli si ugonjwa wa kurogwa, hautokani na uchawi… mtu anazaliwa nao pale anapokuwa amerithi vinasaba kutoka kwa wazazi wetu wote wawili {baba na mama}; Tusiuone ni kitu cha ajabu au ugonjwa wa ajabu ni wa kawaida tu, Mungu keshatupa tunapokea,” anatoa rai. Anasema watu wasiwe na wasiwasi kuhusu ugonjwa huo, huku akishauri “Ukimuona mtoto wako {ana ugonjwa huu} mpeleke hospitali afuatiliwe afya/hali yake ili apatiwe tiba stahiki na elimu ni jambo la msingi hakikisha unampeleka shule kama watoto wengine. Anaongeza “Kuna watu wapo kazini na wana Siko Seli na mimi nilisoma mpaka 'form two' {kidato cha pili} Shule ya Sekondari Miembe Saba. “Zamani shule zilikuwa mbali za sekondari, lakini nilishindwa kuendelea Siko Seli ilinizidi sana; Na nina uchungu sana kwa sababu nilishindwa kumaliza lakini napenda sana, nilitamani niendelee lakini ndiyo hivyo ilinibana sana,” anasema. Shujaa huyo wa Siko Seli anasisitiza “Nawaombeeni dua mlio na matatizo haya mpone, muendelee na kazi zenu vizuri.” “Madaktari wangu wote nawaombea, mnanisikiliza vizuri, mnanitibia vizuri, nashukuru Mungu kwa hilo.”
  16. 16. _ MAISHA, SANAA NA SIKOSELI 03 | MITINDO YA MAISHA SHU AA JARIDA LA J Arafa Na Arafa Said & Emmy Mwita Martin Deus Theo al maarufu Shetani wa mguu mmoja au unaweza kumuita Chiba Kismati ni kijana wa umri wa miaka 36, alizaliwa mpanda Agosti 1985 na alipofika umri wa miaka 2, wazazi wake waligundua kuwa ana sikoseli, taarifa ambazo walizipokea kwa ugumu kutokana na kwamba waliambiwa kuwa ugonjwa huo hauna tiba na mwanao asingeweza kuishi kupita miaka 18. Chiba Kismati anatoa simulizi yake kwa jarida la shujaa kwa kuongeza kuwa, baada ya wazazi wake kuambiwa kuwa asingeweza kupona na kuwa asingeishi kwa zaidi ya miaka 18, walichukua maamuzi ya kugeukia kwenye tiba za Kienyeji ambapo alipelekwa kwa waganga mbalimbali, mikoa tofauti tofauti nchini huku akipewa tiba za madawa ya kienyeji kwa ahadi ya kuwa dawa hizo zingetibu na kuondoa ugonjwa huo wa Sikoseli, anasema kuwa alitumia tiba za ajabu ambazo haziku- saidia bali zilizidi kudhoofisha afya yake, mfano kuna wakati alishauriwa kutumia kinyesi kilichokauka kwa madai ya ku- wa ni tiba ya sikoseli. Haya yote yalitokea kutokana na kw- amba yeye pamoja na wazazi wake hawakuwa na ufahamu na elimu ya sikoseli. Sikoseli iliathiri Maisha yake katika Nyanja kama elimu, ali- shindwa kuendelea na elimu kutokana na kuumwa kwa vipindi vya mda mrefu hadi miezi 6, hivyo ilimlazimu kusitisha elimu yake pale alipofika kidato cha saba ndio ikawa kikomo kwake lakini pia anasema kutokana na kupata vidonda katika mguu am- bacho kilipelekea yeye kupata osteomyelitis na kupelekea kupot- eza mguu kutokana na maambukizi hayo ya mifupa. Baadae aliha- ma kutoka mpanda na kuhamia Dar es salaam ambapo alikua anapata matibabu katika kliniki ya Watoto pale Hospitali ya Taifa Muhimbili. Katika Kukua kwake anasema alihisi kama watu walikua wanampuuza aswa kutokana na kuwa na ulemavu wa mguu, yeye kama msanii wa sanaa ya uigizaji inakua ngumu kupata kazi na pia kutokana na changa- moto za afya na pia kukosa elimu kulipelekea Maisha yake kuwa duni ku- tokana na kukosa kazi na hivyo akaamua kuingia katika tasnia ya uigizaji lakini na huko pia alipata changamoto kutokana na hali yake ya ulemavu. Chiba anakanusha kauli ya kuwa mtu mwenye sikoseli hawezi kuishi miaka zaidi ya 18 kwa kusema kuwa, yeye ana miaka 36 na yupo, anahimiza kikubwa ni kupata elimu na kuzingatia ushauri wa madaktari na lishe bora na kuepuka kazi nzito kupita kiasi; anatoa ushauri kuwa inawez- ekana kuishi miaka zaidi ya miaka 70 pia anahimiza kuwepo semina mkoa kwa mkoa, nchini. Pamoja na kuwa na sikoseli anasema hawezi kukata tamaa kwani anatumia fursa za usanii katika kuelimisha umma kuhusu sikoseli na pia yeye ni baba wa familia na anategemewa kama kichwa cha familia yake hivyo sikoseli haija- mzuia kuwa na Maisha mazuri. Anafuatilia matibabu kwa kuhudhuria kliniki, anazingatia lishe bora pamoja na kan- uni za afya, anashukuru madaktari, jumuiya ya Sikoseli Tanzania. Inaendelea...
  17. 17. _ KUWA MJANJA IJUE SIKOSELI NA KILAZA 03 | MITINDO YA MAISHA SHU AA JARIDA LA J Arafa Na Arafa Said & Emmy Mwita Aboubakar Juma Kilaza, Miaka 35 ni Msanii wa Muziki wa Bongo Flava; Alizaliwa na Sikoseli na kwasababu wazazi walipata elimu kuhusu Sikoseli kwasababu Mama ya- ke alikua ni muuguzi na Baba yake alikua ni muuguzi; kutokana na kwamba wazazi wa- ke walikua na ufahamu wa sikoseli walijitoa katika yeye kupata matibabu, walihangaika katika zahanati mbalimbali kutafuta matibabu na hatimae walifika Hospitali ya Taifa Muhimbili, hapo ndipo alipopata matibabu yake na kuanza kliniki ya sikoseli.Kuwa na Sikoseli hakukufanya ajione tofauti na Watoto wengine, isipokuwa aliku- wa anahitajika kumeza dawa kama Folics Acid na Pen V kila siku na kuhu- dhuria kliniki. Alizidi kukua na kuelewa hadi kupelekea yeye kuwa balozi wa Sikoseli Tanzania. Anasema kwa ujumla hajaathiriwa na sikoseli kabisa kwani Sikoseli kwake imekua kama fursa ya kuwa kijana mwadilifu na kuepu- ka makundi kama ya wavuta bangi na mambo ambayo yanaenda kin- yume na jamii na pia kwakuwa anafanya kazi za sanaa Sikoseli ina- mpa fursa ya kutumia sanaa yake katika kuhamasisha umma kuhusu Sikoseli. Yeye kama msanii anawakilisha na kuelimisha kuhusu si- koseli kwenye nyimbo anazotunga na anapenda kujulikana kwa jina la Mr. Sickle Cell Kila nyimbo anayotoa anaweka jina hilo kama utambulisho. Anasema yeye hawezi kuonekana dhaifu kwa kuwa familia y- ake anaiendesha mwenyewe, anaongeza kusema kuwa Sikos- eli haimfanyi kuwa dhaifu kwani hata bila Sikoseli mtu una- weza kuwa dhaifu.Anahudhuria kliniki na anafurahishwa na hu- duma zinazotolewa lakini pia anaomba serikali pamoja na jamii itambue Si- koseli na washirikiane katika kuboresha na kuimarisha huduma za matiba- bu ya Sikoseli. ...jumuiya ya Sikoseli Tanzania. Inaendelea... Lengo kuu la kuwa na taasisi ya Chiba Kismati ni kutoa fursa na jukwaa kwa wasanii wenye ulemavu na kuondoa matabaka na unyanyapaa uliopo. Yupo kwa ajili ya jamii na kwa lengo la kujitoa kwa jamii. Anategemea kutoa elimu zaidi kupitia taasisi yake ya chiba kismati; kuanzia mikoa ya Arusha, Tanga, Pwani na Zanzibar. Anaomba serikali kuangalia watu wenye sikoseli kwasababu ugonjwa ni wa mda mrefu, anaomba wizara husika iwasaidie katika kup-unguza gaharama za matibabu na kuwajumuisha katika bima. Matarajio yake ni kutumia sanaa yake kufikisha ujumbe kwa wanajamii kuhusu Sikoseli. changamoto ni kukosa miundombinu na rasilimali za kuwezesha kazi hiyo ya uhamasishaji. Ujumbe wake kwa jamii, wasikatishe watu wenye sikoseli tamaa na kusema kuwa hawawezi kuishi mda mrefu kwani yeye ni mfano tosha kuwa ameishi mpaka sasa ana miaka 36, na wengine wengi wenye miaka 60, 70, 90 na kuendelea; Pia anawahasa wanajamii ya sikoseli wasitumie sikoseli kama kudeka na kurahisisha Maisha yao, wafanye kazi zao kwa bidii na vizuri kwani Sikoseli ni ugonjwa kama mengine tu.
  18. 18. SEPTEMBA, MWEZI WA UELEWA WA SIKOSELI. 03 | MITINDO YA MAISHA SHU AA JARIDA LA J Arafa Na Arafa Said & Emmy Mwita Kwa wasiojua na kwa faida ya wanajua sio mbaya tukikumbushana kuwa mwezi wa septemba ni mwezi wa kutoa uelewa na ufahamu juu ya ugonjwa wa Sikoseli duniani. Hivyo Taasisi ya Sickle Cell Disease Patients' of Tanzania kuungana na taasisi na jumuiya kimaifa iliadhimisha siku hiyo kwa kuandaa matukio mbalimbai ya uhamasishaji, uelimishaji na kutoa uelewa juu ya ugonjwa wa sikoseli nchini ikishirikiana na taasisi na washika dau katika sekta ya afya. Kama jumuiya ya wagonjwa wa sikoseli Tanzania na kama wanaharakati na washika dau katika elimu na ufahamu juu ya sikoseli waliandaa Jukwaa la Mashujaa mkoani Pwani, wilaya ya Mkuranga kushirikiana na Hos- pitali ya Wilaya Mkuranga lengo kuu la jukwaa hili likiwa ni kutoa fursa ya majadiliano ya wazi kati ya wanajam- ii wa mkuranga na wataalamu wa afya kuhusu Sikoseli na pia wataalamu waliruhusu wasaa wa maswali na majib- u ambapo changamoto mbalimbali na Imani potofu zinazozunguka ugonjwa wa sikoseli zilijadiliwa na kutolewa majibu sahihi ili kuelimisha wahudhuriaji; pia wahudumu walitoa fursa ya ushauri nasaha kwa mtu mmoja mmoja. Tamasha la Jukwaa la Mashujaa lilifuatiwa na tukio la mnamo tarehe 27, Septemba ambapo taasisi ya SCDPCT iliandaa Upimaji wa Sikoseli bure ikishirikiana na Hospitali ya Wilaya Bagamoyo na Zahanati ya Mwavi iliyopo kata ya fukayosi, mkoani Pwani, upimaji huu uliambatana na ushauri na elimu juu ya sikoseli, pia Sickle Cell Disease Patients' Community of Tanzania kushirikiana na wafadhili wake walifanikiwa kuwafadhili bima Watoto walio chini ya umri wa miaka 16, Bima za afya za NHIF ili kuwasaidia kupata matibabu kwa gharama rahisi na pia kuwahamasisha kuhudhuria kliniki za sikoseli kwa matibabu sahihi ili kuboresha afya zao.Mwezi septemba ulifungwa na kampeni za sauti ya shujaa, ambapo tulipokea video mbalimbali kutoka kwa wanajamii, madaktari na wauguzi, washirika katika sekta ya afya wakitoa elimu na ufahamu juu ya sikoseli kwa wanajamii kupitia njia ya video. Septemba ilinoga, tunakukumbusha na kuhamasisha kuwa usikose kushiriki harakati hizi kwa msimu mwingine wa septemba yani mwaka 2023 kwani yajayo yanafurahisha.
  19. 19. CHANGIA DAMU, OKOA MAISHA. 03 | MITINDO YA MAISHA SHU AA JARIDA LA J Arafa Na Arafa Said & Emmy Mwita Maji ni uhai lakini umewahi kukaa na kufikiri kuwa Damu ni uhai pia? Tukizidi kuhimiza jamii juu ya umuhimu wa kuwa na ufahamu na uelewa wa sikoseli, tungependa kuwakumbusha pia kuwa zaidi ya watu 100,000 uzaliwa na ugonjwa wa sikoseli kila mwaka na Tanzania ni mojawapo kati ya nchi ambazo zinaongoza kwa kuwa na asilimia kubwa ya watu wenye sikoseli duniani. Mgonjwa wa sikoseli anaweza kuhitaji mpaka uniti 100 za damu kwa mwaka kwa ajili ya matibabu ya athari zina- zotokana na ugonjwa huo. Hakuna aliyewahi kupungukiwa kwa kutoa na pia kutoa kutoka moyoni ni zawadi kwa muhitaji; kukosa damu ni mojawapo ya sababu zinazochangia katika kupoteza Maisha kwa wagonjwa wengi wa sikoseli kwasababu kwao damu ni uhai. Unaweza kuwa mwokozi wa Maisha ya wengi kupitia kuchangia damu, unaweza kuokoa Maisha ya mtu aliyepata ajali ya gari, mgonjwa wa saratani anayehitaji damu kwa matibabu yake, zaidi kwa wagonjwa wa sikoseli ambao wanahitaji damu kwa Maisha yao yote ili kuishi. Faida za kuchangia damu ni pamoja na kuchangia damu ni faida kwa moyo wa binadamu kwani kwa kuchangia damu utaweza kuulinda moyo wako na maradhi ya moyo kama vile shinikizo na kuganda kwa damu. Pia utapata kujua hali ya afya yako kupitia vipimo vinavyofanywa kabla ya kutoa damu, pia ni furaha kujua kuwa kupitia ku- changia damu unaokoa Maisha ya wengi ni furaha ya kuishi na kujitoa kwa ajili ya wengine wenye uhitaji kwenye jamii. Kuchangia damu ni bure kabisa, hakuna malipo unaweza kuwa shujaa wa mtu kwa kuchangia dam una kuokoa Maisha yake bure kabisa. Fikiria ni lini mara ya mwisho ulipata kutoa msaada bure bila kulipia gharama yeyote bila kuhitajika shahada yeyote au ubunifu wowote. Mwishoni niseme, unapochangia damu unaongeza mwaka mwingine wa Maisha kwa mpokeaji damu, unatoa siku ingine ya Maisha, siku ingine ya sherehe ya kuzaliwa, zaidi unaongeza siku ingine chini ya usiku wa nyota uliojaa tabasamu na afya, unatoa nafasi nyingine ya kutimiza ndoto na unatoa zawadi nyingine ya Maisha kwa wapendwa wa mpokeaji damu. Hivyo ni kuhimize changia damu, okoa Maisha…Timiza ndoto. Umuhimu wa Uchangiaji Damu
  20. 20. 04 MATANGAZO SHU AA JARIDA LA J Arafa Na Arafa Said & Emmy Mwita MATUKIO NA MAISHA matukionamaisha.blogspot.com Kwa habari na makala za kina kuhusu masuala mbalimbali ya afya na jamii tembelea jukwaa la matukionamaisha.blogspot.com ni akaunti iliyotambuliwa kwa tuzo na Baraza la Habari Tanzania (MCT) mwaka 2021 jukwaa bora katika kuripoti masuala ya afya Tanzania, Aidha Mmiliki wake Veronica Mrema mwaka 2021 alitunukiwa tuzo na Shirikisho la Vyama vya Magonjwa Yasiyoambukiza Afrika Mashariki miongoni mwa waandishi bora wanaoripoti vema.
  21. 21. 04 MATANGAZO SHU AA JARIDA LA J Arafa Na Arafa Said & Emmy Mwita BLACKART
  22. 22. SHU AA MAGAZINE J With Arafa Salim & Emmy Mwita | Meals on Wheel is a private registered enterprise that offers catering services for more than three years now Meals on Wheel works to make any event or meal time a delicious one 04 MATANGAZO
  23. 23. SHU AA MAGAZINE J With Arafa Salim & Emmy Mwita | 04 MATANGAZO +255743222145
  24. 24. SHU AA JARIDA LA J Na Arafa Said & Emmy Mwita Ahsante kwa kusoma Tufuatilie kupitia IG: @sicklecellpatientstz FB: Sickle Cell Disease Patients Community of Tanzania

×